Local,Transfer News,Azam, Al Hilal

Benchi Azam Fc lamchosha Fofana

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 Apr 2026
Benchi Azam Fc lamchosha Fofana

Kipa raia wa Ivory Coast, Issa Fofana, anaonekana kuwa kwenye wakati mgumu ndani ya kikosi cha Azam FC, hali iliyozua tetesi kuwa anaweza kuondoka mwishoni mwa msimu huu.

Kwa mujibu wa taarifa za karibuni, Fofana anafikiria kurejea kwa waajiri wake wa zamani, Al Hilal Omdurman, baada ya kukosa nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza.

Fofana alisajiliwa na Azam FC akiwa na matarajio ya kuwa kipa namba moja, lakini hali imekuwa tofauti baada ya kuongezeka kwa ushindani mkali ndani ya timu.

Kipa Aishi Manula amerejea kwenye kiwango bora, akihusishwa na takwimu nzuri za clean sheets saba katika mechi nane, hali iliyomfanya kuimarisha nafasi yake kikosini.

Pia, chipukizi Zuber Foba ameendelea kuonyesha uwezo wake, na kuongeza ushindani katika nafasi ya ulinzi wa lango.

Kwa mujibu wa vyanzo vya karibu na mchezaji huyo, Al Hilal Omdurman wanafuatilia kwa karibu hali ya Fofana na wanaweza kuchukua hatua ya kumrudisha endapo Azam FC wataamua kumtoa katika dirisha lijalo la usajili.

Fofana aliwahi kufanya vizuri akiwa Sudan wakati Al Hilal ikiwa chini ya kocha Florent Ibenge ambaye ndiye aliyependekeza usajili wake kujiunga na Azam Fc lakini amekabiliwa ushindani mkali kutoka kwa walinda lango wa ndani.

Bado hakuna taarifa rasmi kutoka kwa Azam FC kuhusu mustakabali wa kipa huyo, lakini dalili zinaonyesha kuwa kwenye usajili wa dirisha lijalo huenda wakamruhusu mlinda lango huyo kusaka changamoto sehemu nyingine.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
9h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
12h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
18h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’