Local,Normal News,International,Normal News,Ballon d’Or, UEFA, World Cup

Vigezo Rasmi Ballon d’Or 2026 Vyatangazwa, UCL na Kombe la Dunia Kuwa Muhimu Zaidi

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
β€’
10 Apr 2026
Vigezo Rasmi Ballon d’Or 2026 Vyatangazwa, UCL na Kombe la Dunia Kuwa Muhimu Zaidi

Jarida la France Football limetangaza rasmi mfumo mpya wa tathmini kwa tuzo ya Ballon d’Or ya mwaka 2026, likibainisha vigezo vinne vikuu vitakavyotumika kuwachuja wachezaji bora duniani.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wagombea wote watapimwa kwa kuzingatia mambo yafuatayo:

Kwanza ni mafanikio ya pamoja na mataji, ambapo ubingwa katika ngazi ya klabu na timu ya taifa utaendelea kuwa msingi mkuu wa ushindani wa tuzo hiyo.

Pili ni kiwango binafsi cha mchezaji, ubora wake uwanjani, uwezo wa kubadilisha matokeo ya mechi na mchango wake wa moja kwa moja katika mafanikio ya timu msimu mzima.

Tatu ni nidhamu na uungwana, ambapo tabia njema ndani na nje ya uwanja itakuwa sehemu muhimu ya tathmini ya mchezaji.

Nne ni uwezo wa kung’ara katika mechi kubwa, hasa fainali na hatua za mtoano, ambapo wachezaji hupimwa zaidi kwa namna wanavyobeba timu katika nyakati za presha kubwa.

Aidha, katika toleo la mwaka 2026, msisitizo mkubwa umewekwa kwa mashindano makubwa zaidi duniani, ukiwemo UEFA Champions League na FIFA World Cup.

Imeelezwa wazi kuwa ni wachezaji watakaoonyesha kiwango cha kipekee katika mashindano hayo mawili pekee watakaokuwa na nafasi halisi ya kutwaa tuzo hiyo kubwa zaidi binafsi katika soka.

More Stories

Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
1h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
1h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
2h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
2h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
10h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
14h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
15h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
17h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
17h ago
READ MORE β†’