Klabu ya Simba SC imeibuka tena ikihusishwa na harakati za kumwania kipa namba moja wa timu ya taifa ya Nigeria Stanley Nwabali, kuelekea msimu wa 2026/2027.
Nwabali anatajwa kuwa ni chaguo la Kocha Mkuu wa Simba Steve Barker ambaye alipendekeza usajili wake ambapo baada ya mchakato wa kumsajili kukwama, ndio Wekundu hao wa Msimbazi wakamsajili Djibrilla Kassali.





