Leo mabingwa watetezi wa michuano ya kombe la CRDB Yanga watashuka uwanja wa KMC Complex kuikabili TMA Stars katika mchezo wa kusaka tiketi ya kutinga robo fainali ya michuano hiyo. Mtanange huo unatarajiwa kupigwa saa 12:30 kwa saa za Afrika Mashariki.
Yanga itaingia kwenye mchezo huku ikiwa na rekodi ya aina yake katika michuano hiyo inayodhaminiwa na benki ya CRDB.
Mara ya mwisho Yanga kupoteza mchezo wa Kombe la Shirikisho nchini Tanzania ilikuwa Julai 26,2021 kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Simba uliochezwa dimba la Lake Tanganyika Mkoani Kigoma ambapo Simba waliifunga Yanga bao 1-0 lililofungwa na Taddeo Lwanga dakika ya 79' ya mchezo na kuipa Simba ubingwa.
Tangu mchezo huo mpaka sasa Yanga haijawahi kupoteza mchezo wowote ule kwenye michuano hiyo. zikiwa zimepita siku 1,721 awa na wiki 245 na siku 6.
Ni sawa na miaka 4, miezi 8 na siku 17 ambayo pia ni sawa na masaa 41,304. Leo Wananchi watakuwa wakiisaka tiketi ya robo fainali mbele ya TMA Stars ambayo yawezekana ikaonekana ni timu nyepesi lakini hawajafika hatua ya 16 bora kwa bahati mbaya.Β
Je Wananchi wataendeleza ubabe wao katika michuano hiyo au ule msemo wa 'mende kudondosha kabati' unaweza kutimia?