Local,Normal News,Simba, Dodoma

Barker Afichua Mipango Simba Kuizima Dodoma Jiji 16 Bora Kombe la CRDB

Joel JJ By Joel JJ
11 Apr 2026
Barker Afichua Mipango Simba Kuizima Dodoma Jiji 16 Bora Kombe la CRDB

Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, amesema atafanya mabadiliko machache ya kiufundi katika kikosi chake kuelekea mchezo wa hatua ya 16 bora ya Kombe la CRDB dhidi ya Dodoma Jiji, unaotarajiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Barker amesema mabadiliko hayo yanalenga kuongeza ubunifu wa timu katika kutengeneza nafasi za mabao, hasa kutokana na changamoto ya ukame wa mabao iliyojitokeza katika michezo ya hivi karibuni.

Akizungumza kuelekea mchezo huo, Barker alikiri kuwa timu yake imekuwa ikipata nafasi nyingi lakini imekosa umakini wa kuzitumia ipasavyo.

“Mechi ya mwisho tuliyocheza dhidi ya Dodoma Jiji nafikiri tulikuwa na kiwango bora, haikuwa bahati upande wetu hatukuweza kufunga bao lolote,” alisema.

Kocha huyo aliongeza kuwa hali hiyo haijitokezi kwa mara ya kwanza, akibainisha kuwa Simba SC pia haikufanikiwa kufunga katika mechi mbili za Ligi Kuu Tanzania Bara zilizopita.

“Pia tumecheza mechi mbili za ligi kuu pasipo kufunga bao, tunafahamu changamoto inayotukabili na tunafanya kazi kubwa kwenye uwanja wa mazoezi,” alifafanua.

Barker amesema tayari benchi la ufundi linafanyia kazi marekebisho ya kimkakati yatakayosaidia kuongeza ufanisi wa safu ya ushambuliaji na kuimarisha uwezo wa kutengeneza nafasi.

“Tunahitaji kutengeneza nafasi zaidi ili tuweze kufunga magoli, hivyo tutafanya mabadiliko machache ya kimbinu ambayo naamini yatatupa wigo mpana wa kutengeneza nafasi na kufunga mabao,” alisema.

Mchezo huo unatarajiwa kuwa wa ushindani mkubwa kutokana na umuhimu wake katika hatua ya mtoano, huku kila timu ikiwania nafasi ya kutinga robo fainali ya michuano hiyo

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
47m ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
5h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
5h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
7h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
11h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
13h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
14h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →