International,Normal News,Local, Chelsea

Basi la timu lavamiwa na majambazi Ghana, mchezaji auawa

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Apr 2026
Basi la timu lavamiwa na majambazi Ghana, mchezaji auawa

Tasnia ya soka nchini Ghana imekumbwa na msiba mzito kufuatia kifo cha mchezaji chipukizi Dominic Frimpong, aliyefariki dunia baada ya kushambuliwa kwa risasi katika tukio la ujambazi lililolenga basi la timu yake.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari vya kimataifa, tukio hilo lilitokea Jumapili, Aprili 12, 2026, wakati timu ya Berekum Chelsea ikirejea kutoka mchezo wa Ligi Kuu Ghana dhidi ya Samartex.

Inaelezwa kuwa watu wenye silaha walivamia basi hilo njiani na kuanza kufyatua risasi, hali iliyosababisha taharuki kubwa miongoni mwa wachezaji na viongozi wa timu hiyo. Katika tukio hilo, Frimpong alipigwa risasi kichwani na baadaye alifariki dunia alipokuwa akipatiwa matibabu hospitalini.

Frimpong, aliyekuwa na umri wa miaka 20, alikuwa akiichezea Berekum Chelsea kwa mkopo akitokea Aduana FC. Katika msimu huu, alikuwa amecheza mechi kadhaa na kuonyesha kiwango kizuri kilichomfanya kuwa miongoni mwa wachezaji wanaochipukia nchini humo.

Shirikisho la Soka Ghana (GFA) limelaani tukio hilo na kutoa salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu, klabu pamoja na wadau wa soka nchini humo.

Tukio hilo pia limeibua hofu kuhusu usalama wa timu za soka wakati wa safari za kwenda na kurejea kwenye mechi za ligi, huku mamlaka zikiahidi kufanya uchunguzi na kuwabaini wahusika wa shambulio hilo.

Kifo cha Frimpong kimeacha pengo kubwa katika soka la Ghana, huku mashabiki na wadau mbalimbali wakiendelea kutoa pole na kutaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya wahusika wa tukio hilo.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
10h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
12h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
19h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’