International,Normal News,Barcelona, UEFA

Yamal na ujumbe kwa mashabiki wa Barca

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
15 Apr 2026
Yamal na ujumbe kwa mashabiki wa Barca

Nyota chipukizi wa FC Barcelona, Lamine Yamal, ametuma ujumbe mzito na wa kihisia kwa mashabiki wa klabu hiyo kufuatia kuondolewa kwenye UEFA Champions League.

Katika ujumbe wake, Yamal alieleza maumivu makubwa aliyoyapata baada ya ndoto ya kutwaa taji hilo kufifia:

“Kwa kweli sina maneno ya kuelezea ninavyohisi kwa sasa. Nimekaa gizani, bado siamini kwamba imeisha. Kwa mashabiki wetu — naomba radhi sana. Tumewaangusha tena, na huu ni uchungu nitakaoubeba kila usiku hadi tutakapolirekebisha hili. Mnatusafiria, mnashangilia, mnalia kwa ajili yetu, lakini usiku huu tumewapa maumivu zaidi tu.”

Yamal aliweka wazi kuwa ndoto yake kubwa tangu alipojiunga na akademi ya La Masia ni kuirejesha Barcelona kileleni mwa Ulaya, na kushindwa kufanikisha hilo kwa sasa kunamuumiza sana:

“Nimekuwa nikiota kuirudisha nyumbani hii kombe tangu siku yangu ya kwanza La Masia. Ni kitu pekee ninachotaka. Kuiona ikitupita hivi ni kama ndoto mbaya ambayo siwezi kuamka.”

Hata hivyo, kijana huyo mwenye umri mdogo aliahidi kutokata tamaa, akisisitiza kuwa ataendelea kupambana hadi kufanikisha ndoto hiyo:

“Nisikilize sasa: sitaacha kamwe. Haijalishi itachukua miaka mingapi au nitahitaji kujitoa kiasi gani — sitapumzika hadi kombe hilo lirudi Barcelona mahali linapostahili. Maisha yangu, roho yangu na kila jasho langu ni kwa ajili ya klabu hii. Tutarudi tena. Na nawaahidi hilo.”

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
4h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
9h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
11h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
11h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
15h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
17h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
18h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →