Local,Normal News,Yanga, Simba, Azam, JKT, Singida BS

Yanga yafungua gap la Alama 5 baada ya viporo kukamilika

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Apr 2026
Yanga yafungua gap la Alama 5 baada ya viporo kukamilika

Baada ya kukamilika kwa mechi za viporo za Ligi Kuu NBC, sasa pazia la mzunguko wa 18 limefungwa rasmi huku baadhi ya timu zikianza tayari harakati za mzunguko wa 19.

Matokeo ya leo yameshuhudia Simba SC ikiibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Fountain Gate FC, ushindi ambao umeifanya iendelee kusalia katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi. Hata hivyo, ushindi huo haujatosha kuziba pengo dhidi ya vinara wa ligi, Yanga SC.

Yanga wameendelea kushikilia kilele cha msimamo kwa kuongoza na alama 44 baada ya kucheza mechi 18, wakiacha pengo la alama tano dhidi ya watani zao wa jadi Simba wenye alama 39 baada ya idadi sawa ya mechi. Tofauti hiyo sasa inaiweka Yanga katika nafasi nzuri ya kutetea ubingwa kwa msimu wa tano mfululizo kama watafanya vizuri katika mechi 12 zilizobaki.

Katika nafasi ya tatu, Azam FC wanaendelea kujikita wakiwa na alama 34 baada ya mechi 18, huku JKT Tanzania wakishika nafasi ya nne kwa alama 29, pia baada ya kucheza mechi 18.

Kwa mtazamo wa ushindani wa ubingwa, unaweza kusema safari ya Yanga kuelekea kutwaa ubingwa wa tano mfululizo iko mikononi mwao.

Katika mechi 12 zilizobaki, Wananchi watahitaji kushinda angalau mechi 10 ili kujihakikishia ubingwa huo, huku wakilazimika kuepuka kupoteza mechi muhimu dhidi ya wapinzani wao wakuu Simba na Azam FC.

Kadri ligi inavyoelekea ukingoni, presha inaendelea kuongezeka, na kila pointi itakuwa na uzito mkubwa katika kuamua nani ataibuka bingwa wa msimu huu wa 2025/2026.

More Stories

Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
4h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
4h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
6h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
10h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
12h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
13h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
1d ago
READ MORE β†’