Local,Normal News,TRA, Pamba

TRA United yaichapa Pamba Jiji 1-0, yapanda nafasi ya 6

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Apr 2026
TRA United yaichapa Pamba Jiji 1-0, yapanda nafasi ya 6

Klabu ya TRA United imeendelea kuonyesha makali yake nyumbani baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Pamba Jiji FC katika dimba la Sheikh Amri Abeid.

Katika mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa, Chanda Chewe akifunga bao pekee la ushindi katika dakika ya 60. Bao hilo lilitosha kabisa kuwapa TRA United alama tatu muhimu mbele ya mashabiki wao.

Pamba Jiji ilijaribu kusaka bao la kusawazisha kwa kushambulia mara kadhaa, lakini safu ya ulinzi ya TRA United ilikuwa imara na haikutoa nafasi rahisi hadi mwisho wa mchezo.

Kwa ushindi huo, TRA United imefikisha pointi 27 na kupanda hadi nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara.

Kwa upande wa Pamba Jiji, kipigo hicho kimewaacha na pointi 26 na kushuka hadi nafasi ya saba, hali inayoongeza presha kwa wakulima hao wa Pamba katika mpango wao wa kusaka nafasi za juuu kwenye msimamo wa ligi.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
3h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
7h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
8h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
10h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
10h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
14h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
16h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’