Klabu ya TRA United imeendelea kuonyesha makali yake nyumbani baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Pamba Jiji FC katika dimba la Sheikh Amri Abeid.
Katika mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa, Chanda Chewe akifunga bao pekee la ushindi katika dakika ya 60. Bao hilo lilitosha kabisa kuwapa TRA United alama tatu muhimu mbele ya mashabiki wao.





