International,Normal News,Barcelona

Messi anunua klabu Hispania

Joel JJ By Joel JJ
17 Apr 2026
Messi anunua klabu Hispania

Gwiji wa soka duniani, Lionel Messi, amefungua ukurasa mpya katika maisha yake nje ya uwanja baada ya kuthibitishwa kuwa mmiliki mpya wa klabu ya Hispania, UE Cornellà.

Taarifa kutoka Hispania zinaeleza kuwa Messi amenunua asilimia 100 ya hisa za klabu hiyo inayoshiriki ligi ya daraja la tano nchini Hispania .

Klabu hiyo yenye makazi yake Catalonia, karibu na jiji la Barcelona, imeeleza kuwa ujio wa Messi unaashiria mwanzo wa enzi mpya yenye malengo ya kukuza vipaji vya vijana, kuimarisha miundombinu ya klabu, na kujenga mafanikio ya muda mrefu.

Hatua hiyo pia inaonekana kuimarisha zaidi uhusiano wa Messi na eneo la Catalonia, ambako alijijengea jina kubwa akiwa mchezaji wa FC Barcelona kwa miaka mingi.

Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali, uwekezaji huo si wa kifedha pekee, bali unaambatana na mpango wa kimkakati wa kuendeleza soka la vijana na kuifanya klabu kuwa imara kiushindani na kiutawala kwa muda mrefu.

UE Cornellà inajulikana kwa historia yake ya kukuza vipaji, ikiwa imewahi kutoa wachezaji waliokuja kung’ara Ulaya kama Jordi Alba na David Raya.

Hatua ya Messi inaongeza orodha ya mastaa wa soka wanaoingia kwenye umiliki wa vilabu, ikiwa ni maandalizi ya maisha baada ya kucheza na njia ya kuacha urithi mkubwa zaidi ndani ya mchezo huo.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
4h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
9h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
11h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
11h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
15h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
17h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →