Local,Normal News,Azam, JKT

Azam Fc yaifumua JKT Tanzania 3-0

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Apr 2026
Azam Fc yaifumua JKT Tanzania 3-0

Azam FC imeibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Ijumaa, Aprili 17, 2026, kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Azam FC ilipata ushindi wake katika kipindi cha pili, Japhet Kitambala akifungua ukurasa wa mabao kabla ya Iddy Nado kufunga mabao mawili yaliyokamilisha ushindi huo mnono.

Kipindi cha kwanza cha mchezo kilimalizika bila kufungana (0-0), huku timu zote zikionyesha ushindani mkali na tahadhari kubwa katika safu za ulinzi.

Baada ya mapumziko, Azam FC walirudi uwanjani kwa kasi na kushambulia kwa nguvu, hatua iliyowawezesha kupata bao la uongozi kupitia Kitambala dakika za mwanzo za kipindi cha pili.

Feisal Salum 'Fei Toto' alikuwa tishio kwa JKT Tanzania akitoa pasi za mabao mawili na sasa akiongoza orodha ya vinara wa asisti akifikisha saba.

JKT Tanzania walijaribu kufanya mashambulizi ya kusawazisha lakini walikosa umakini katika umaliziaji pamoja na kukutana na ulinzi imara wa Azam FC.

Ushindi huo unaifanya Azam FC izidi kujiimarisha kwenye nafasi ya tatu ikifikisha alama 37, alama mbili nyuma ya Simba inayoshika nafasi ya pili.

Kipigo kwa JKT Tanzania kimewashusha hadi nafasi ya tano kwenye msimamo wa ligi nyuma ya Singida BS wakiwa na alama sawa 29 tofauti ikiwa uwiano wa mabao

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
9h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
12h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
18h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’