Local,Transfer News,Yanga, Simba

Simba yashtukia, yaanza mchakato wa kumbakisha Mwalimu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Apr 2026
Simba yashtukia, yaanza mchakato wa kumbakisha Mwalimu

Klabu ya Simba SC imeanza mchakato wa kumbakisha mshambuliaji wake Suleiman Mwalimu ambaye mkataba wake wa mkopo unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu.

Kwa mujibu wa makubaliano ya awali, Mwalimu atarejea katika klabu yake mama ya Wydad AC mwezi Juni mara baada ya mkataba wake wa mkopo kumalizika.

Hata hivyo, uongozi wa Simba umeanza mapema harakati za kuhakikisha mshambuliaji huyo anabaki Msimbazi kwa msimu mwingine, kutokana na mchango wake mkubwa ndani ya kikosi.

Taarifa zinaeleza kuwa klabu hiyo inapendelea ama kumsajili moja kwa moja au kumwongezea mkopo mwingine, endapo dili la ununuzi wa moja kwa moja litashindikana.

Hatua hiyo imechochewa na kiwango bora cha Mwalimu msimu huu, ambapo amekuwa mchezaji tegemeo katika safu ya ushambuliaji.

Mshambuliaji huyo, amekuwa na msimu mzuri akiwa kinara wa mabao ndani ya Simba, akifunga jumla ya mabao 6 katika Ligi Kuu ya NBC.

Kocha wa Simba, Steve Barker, anamtegemea Mwalimu katika mfumo wake wa ushambuliaji, akimuona kama sehemu muhimu ya β€œproject” ya msimu ujao.

Inaelezwa mpango wa Simba ni kuhakikisha wanakamilisha dili hilo mapema ili kuepuka ushindani kutoka kwa klabu nyingine zinazoweza kuvutiwa na kiwango cha mchezaji huyo.

Kwa mujibu wa taarifa, hatua hii imechukuliwa mapema pia kutokana na taarifa zinazoibuka kwamba mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga nao wamekuwa na mawasiliano na Wydad wakilenga kumsajili Mwalimu.

Kitendo cha Mwalimu juzi kuonekana uwanja wa KMC Complex wakati Yanga ikichuana na Mbeya City kwenye mchezo wa ligi kuu ya NBC kimeibua mijadala mingi mitandaoni juu ya mustakabali wake.

Hata hivyo nyota huyo alitumia muda wake wa mapumziko akiambatana na marafiki zake kwenda kushuhudia mchezo huo. Kocha wa Simba Steve Barker aliwapa wachezaji wake mapumziko baada ya kurejea Dar kutoka Arusha walikocheza mchezo wa ligi kuu dhidi ya Fountain Gate

More Stories

Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
4h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
4h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
6h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
6h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
10h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
12h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
13h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
1d ago
READ MORE β†’