Local,Normal News,Azam

Fei Toto namba zake zinazungumza Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Apr 2026
Fei Toto namba zake zinazungumza Ligi Kuu

Kiungo wa Azam FC, Feisal Salum maarufu kama 'Fei Toto', ameendelea kuwa nguzo muhimu ya timu hiyo akionyesha kiwango cha juu katika Ligi Kuu Bara.

Ijumaa usiku, Fei Toto aliiongoza Azam Fc kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Tanzania mchezo wa ligi kuu ya NBC akitoa asisti 2

Msimu huu wa 2025/26, Fei Toto ameshiriki moja kwa moja katika mabao 14 mpaka sasa, akifunga mabao 7 na kutoa assisti 7.

Fei Toto amekuwa na mwendelezo mzuri katika misimu mitatu aliyoitumikia Azam Fc.

Msimu wa 2024/25, Fei Toto aliongoza kwa assisti katika Ligi Kuu Bara baada ya kuisaidia Azam FC kufanikisha mabao 17 (mabao manne na assisti 13).

Aidha, mwaka 2024 ulikuwa wa dhahabu kwa nyota huyu, baada ya kuisaidia timu yake kufanikisha mabao 27 (mabao 15 na assisti 12), akimzidi Stephane Aziz Ki wa Yanga aliyefanikisha mabao 21 (mabao 12 na assisti tisa).

Msimu wa 2023/24, Fei Toto alifunga mabao 19 ya Ligi Kuu Bara, akishika nafasi ya pili kwa ufungaji miongoni mwa wachezaji, nyuma ya Aziz Ki aliyefunga 21. Pia, alijitokeza katika Kombe la Shirikisho (FA), akiisaidia Azam FC kufika fainali kwenye New Amaan Complex Juni 2, 2024, ambapo walipoteza kwa penalti 6-5 dhidi ya Yanga baada ya sare ya 0-0 ndani ya dakika 120.

Kwa misimu mitatu mfululizo, Fei Toto ameonyesha kuwa si tu mchezaji mwenye ubora wa kipekee, bali pia ni kiungo muhimu katika kikosi cha Azam FC.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
6h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’