International,Normal News,Manchester City, arsenal, EPL, Local

Arsenal yachapika Etihad, Mbio za ubingwa EPL ni kama zimeanza upya

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
β€’
19 Apr 2026
Arsenal yachapika Etihad, Mbio za ubingwa EPL ni kama zimeanza upya

Klabu ya Manchester City imeibuka na ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Arsenal katika mchezo wa Premier League uliochezwa katika dimba la Etihad, matokeo yaliyoitikisa kwa kiasi kikubwa mbio za ubingwa wa msimu huu.

Katika mchezo huo, City walipata mabao kupitia Rayan Cherki na Erling Haaland, huku bao la kufutia machozi la Arsenal likifungwa na Kai Havertz.

Ushindi huo unaongeza presha kwa Arsenal, ambao wamekuwa wakiongoza ligi kwa muda mrefu lakini sasa wanaonyesha dalili za kushuka kiwango. Katika michezo sita ya hivi karibuni, Gunners wameshinda mara moja pekee na kupoteza mara nne hali inayotia shaka juu ya uwezo wao wa kudumisha ubora hadi mwisho wa msimu.

Kwa upande wa Manchester City, ushindi huo unawapa nguvu mpya katika mbio za ubingwa, huku wakibaki na mechi nyingi zaidi ya Arsenal hali inayoweza kuwapa faida muhimu katika wiki za mwisho za ligi.

Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, ameendelea kusisitiza kuwa mbio za ubingwa bado hazijaamuliwa, akieleza kuwa timu yake bado inaongoza kwa tofauti ya pointi na kuna mechi kadhaa muhimu zilizosalia.

Hata hivyo, matokeo ya mchezo huo yamebadilisha mwelekeo wa ushindani, huku Manchester City wakionekana kuimarika zaidi katika kipindi hiki muhimu cha msimu.

Kwa sasa, mbio za ubingwa wa Premier League zinaingia katika hatua ya mwisho yenye ushindani mkali, ambapo kila pointi inaweza kuamua nani atakayenyanyua taji mwishoni mwa msimu.

More Stories

Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
11m ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
7h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
12h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
12h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
14h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
14h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
18h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
20h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
21h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’