Klabu ya Manchester City imeibuka na ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Arsenal katika mchezo wa Premier League uliochezwa katika dimba la Etihad, matokeo yaliyoitikisa kwa kiasi kikubwa mbio za ubingwa wa msimu huu.
Katika mchezo huo, City walipata mabao kupitia Rayan Cherki na Erling Haaland, huku bao la kufutia machozi la Arsenal likifungwa na Kai Havertz.





