International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne April 21 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Apr 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne April 21 2026

Soko la usajili linaendelea kushika kasi huku vilabu vikubwa vikifanya maamuzi muhimu kabla ya dirisha la majira ya kiangazi. Hizi hapa ni tetesi moto za leo kutoka vyanzo mbalimbali vya michezo:

Newcastle Wako Tayari Kumuza Anthony Gordon

Kwa mujibu wa The Times, Newcastle United wako tayari kumuuza Anthony Gordon kwenda Bayern Munich iwapo watapata ofa ya pauni milioni 75.

Manchester United Wamuwania Tchouameni

Ripoti kutoka The Telegraph zinaeleza kuwa Manchester United wanafuatilia kwa karibu hali ya Aurelien Tchouameni ndani ya Real Madrid, wakipanga kusajili viungo wawili msimu huu wa joto.

Liverpool Wamuweka Diomande Kama Mrithi wa Salah

Kwa mujibu wa Florian Plettenberg wa Sky Sport Germany, Liverpool FC wamemuweka Yan Diomande kama chaguo kuu la kuchukua nafasi ya Mohamed Salah.

Mustakabali wa Cristian Romero

CaughtOffside linaripoti kuwa Cristian Romero anawindwa na Atletico Madrid huku hatma yake ndani ya Tottenham Hotspur ikiwa haijulikani.

Curtis Jones Aweza Kuondoka Liverpool

Kwa mujibu wa Football Insider, Curtis Jones haridhishwi na muda mdogo wa kucheza ndani ya Liverpool na anaweza kuondoka majira ya joto.

Bastoni Aipendelea Barcelona

Ripoti kutoka Mundo Deportivo zinaeleza kuwa Alessandro Bastoni yuko tayari kuondoka Inter Milan lakini anaipendelea FC Barcelona kuliko Manchester City au Liverpool FC.

Liverpool Wamuwania Enzo Le Fee

Kwa mujibu wa Teamtalk, Liverpool FC ni miongoni mwa vilabu vinavyomuwania Enzo Le Fee kutoka Sunderland AFC.

Chelsea Wamwasiliana na Wakala wa Adeyemi

Ripoti za Fussballdaten zinaonyesha kuwa Chelsea FC wamewasiliana na wakala wa Karim Adeyemi wa Borussia Dortmund.

Everton Wamkaribia Hayden Hackney

Kwa mujibu wa Teamtalk, Everton FC wanaongoza mbio za kumsajili Hayden Hackney kutoka Middlesbrough FC.

John Stones Aweza Kuondoka Man City

Fabrizio Romano anaripoti kuwa John Stones anaweza kuondoka Manchester City kama mchezaji huru majira ya joto.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
44m ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
5h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
5h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
7h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
11h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
13h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
14h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’