Local,Normal News,Azam, KVZ

Ibenge aitaka nusu fainali kombe la Muungano

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Apr 2026
Ibenge aitaka nusu fainali kombe la Muungano

Kocha Mkuu wa Azam Fc Florent Ibenge amekiri kuwa mchezo wa robo fainali kombe la Muungano dhidi ya KVZ anatarajia utakuwa mgumu hata hivyo lengo lake ni kuona wanashinda mchezo huo na kutinga nusu fainali ya michuano hiyo.

Ibenge amesema KVZ ni moja ya timu bora visiwani Zanzibar ikiwa kileleni mwa msimamo wa ligi hivyo anatarajiwa hawatakuwa na kazi nyepesi dhidi yao hapo kesho.

"Sisi tunafanya maandalizi yetu tukiwa na lengo la kushinda na kusonga mbele hatua ya nusu fainali."

"Bila ya kuwakosea heshima wapinzani wetu, natambua wana timu nzuri kwa sasa unaweza kusema ndio timu hapa visiwani Zanzibar lakini nisema tu sisi tunataka kufuzu hatua inayofuata," alisema.

Azam Fc walitua visiwani Zanzibar jana leo wakitarajiwa kukamilisha maandalizi yao tayari kwa mtanange dhidi ya KVZ ambao unatarajiwa kuwa na upinzani mkali.

Endapo Azam Fc itafuzu hatua ya nusu fainali, inaweza kukutana na mabingwa watetezi wa michuano hiyo Yanga ambao wao wanacheza leo dhidi ya Muembe Makumbi katika mchezo wa kwanza wa robo fainali

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
9h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
12h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
18h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’