International,Normal News,Yanga, Belouizdad, Local

Ramovic, Belouizdad wafikishana FIFA

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Apr 2026
Ramovic, Belouizdad wafikishana FIFA

Kocha wa zamani wa klabu ya CR Belouizdad, Sead Ramovic, ameripotiwa kuwasilisha malalamiko katika shirikisho la soka duniani FIFA, kufuatia mgogoro wa kimkataba kati yake na klabu hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa nchini Algeria, Ramovic amechukua hatua hiyo baada ya kutokea mvutano unaohusiana na masuala ya utekelezaji wa mkataba wake, ikiwemo madai ya kucheleweshwa au kutotekelezwa kwa baadhi ya masharti ya kifedha.

Inaelezwa kocha huyo na nmaafisa wake katika benchi la ufundi wana madai ya malimbikizo ya mishahara kwa miezi minne.

Kocha huyo, ambaye amewahi pia kuinoa Young Africans SC kabla ya kuhamia Algeria, pia anadaiwa kuwa katika mgogoro wa kiuongozi uliodumu kwa muda na uongozi wa CR Belouizdad.

Ramovic alitua Belouizdad msimu uliopita baada ya kuachana na Yanga ambapo katika msimu mmoja alioinoa timu hiyo, mafanikio makubwa ni kuwafikisha nusu fainali ya kombe la Shirikisho (CAFCC) msimu huu.

Hata hivyo hakushuhudia mechi za nusu fainali kwani tayari uongozi wa Belouizdad ulikuwa umemsimamisha kabla ya kutangaza kumfuta kazi hivi karibuni.

More Stories

Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
4h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
4h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
6h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
10h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
12h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
13h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
1d ago
READ MORE β†’