Local,Normal News,Yanga, Makumbi

Yanga yatinga nusu fainali Kombe la Muungano kwa kishindo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Apr 2026
Yanga yatinga nusu fainali Kombe la Muungano kwa kishindo

Mabingwa watetezi, Yanga, wameonyesha ubabe wao kwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la Muungano baada ya ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Muembe Makumbi. Mchezo huo ulipigwa katika dimba la New Amaan Complex visiwani Zanzibar.

Kuanzia dakika za mwanzo, Yanga walionekana kuwa na dhamira ya kutetea ubingwa wao, wakilitawala dimba kwa kiwango cha juu na kuonyesha utofauti mkubwa wa ubora dhidi ya wapinzani wao.

Alikuwa mshambuliaji Prince Dube aliyefunga mabao mawili muhimu, huku Shekhan Khamis akiongeza bao moja na bao lingine likiwa la kujifunga kwa upande wa Muembe Makumbi.

Muembe Makumbi walionekana kuzidiwa kwa kiasi kikubwa, wakishindwa kabisa kuifikia safu ya ulinzi ya Yanga au kumpa presha yoyote kipa Djigui Diarra. Ilikuwa ni mechi ya upande mmoja kwa muda mwingi, jambo lililoonyesha ubora na maandalizi ya Yanga katika mashindano haya.

Kwa upande wa tuzo binafsi, Shekhan Khamis aling’ara na kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa mechi, huku Mudathir Yahya akiondoka na tuzo ya nidhamu kutokana na mwenendo wake mzuri uwanjani.

Sasa macho ya Yanga yanaelekezwa katika hatua inayofuata, wakisubiri mshindi wa robo fainali nyingine kati ya KVZ na Azam FC. Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Jumatano na utaamua nani atakayepepetana na Yanga katika nusu fainali.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
49m ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
5h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
5h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
7h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
11h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
13h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
14h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’