Local,Normal News,Mbeya

Mayanga apewa fupa la Mbeya City

Joel JJ By Joel JJ
22 Apr 2026
Mayanga apewa fupa la Mbeya City

Klabu ya Mbeya City imemteua Salum Mayanga kuwa kocha mkuu mpya kufuatia kuondoka kwa Mecky Maxime na benchi lake la ufundi. Uamuzi huu unakuja katika kipindi kigumu kwa timu hiyo, ambayo inapambana kujinasua kwenye hatari ya kushuka daraja.

Mayanga si mgeni ndani ya kikosi hicho cha “Wagonga Nyundo”. Aliwahi kuinoa timu hiyo zamani wakati ikishiriki Ligi ya Championship (daraja la kwanza), jambo linaloipa faida klabu kutokana na uzoefu wake na uelewa wa mazingira ya timu. 

Hali ya Ligi Kuu ya NBC kwa Mbeya City si ya kuridhisha. Timu hiyo inashika nafasi ya 14 ikiwa na alama 17 baada ya michezo 19, nafasi inayoiweka karibu kabisa na mstari wa kushuka daraja. Presha ni kubwa, na macho yote sasa yanaelekezwa kwa Mayanga kuibadilisha hali hiyo kabla mambo hayajawa mabaya zaidi.

Mtihani wa kwanza kwa kocha huyo mpya utakuwa dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo unaotarajiwa kuchezwa Alhamisi, Aprili 30, 2026. Mchezo huo utafanyika katika dimba la Tanzanite Kwaraa Stadium kuanzia saa 10:15 jioni.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
46m ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
5h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
5h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
7h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
11h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
13h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
14h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →