Local,Normal News,Yanga, Azam

Yanga na Azam FC kukutana nusu fainali Muungano Cup

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Apr 2026
Yanga na Azam FC kukutana nusu fainali Muungano Cup

Mashabiki wa soka wanatarajia burudani ya hali ya juu baada ya Yanga SC na Azam FC kufuzu hatua ya nusu fainali ya Kombe la Muungano. Mchezo huo mkubwa utapigwa Jumamosi, April 25 katika dimba la New Amaan Complex, Zanzibar.

Azam FC ilitinga nusu fainali Jumatano usiku baada ya kuichapa KVZ mabao 2-0 katika mchezo wa pili wa robo fainali, ikionyesha uimara mkubwa hasa katika safu ya ushambuliaji na nidhamu ya kujilinda.

Kwa upande wa Yanga, wao walikuwa wa kwanza kukata tiketi ya nusu fainali baada ya kuifunga Muembe Makumbi mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa Jumanne. Yanga walionyesha kiwango cha juu, wakitawala mchezo kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Sasa macho yote yanaelekezwa Zanzibar, ambapo dabi ya Dar es Salaam itahamia visiwani. Mchezo huu unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na historia ya timu hizi mbili pamoja na ubora wa vikosi vyao.

Je, Yanga wataendelea na makali yao au Azam FC watabadili upepo na kukata tiketi ya fainali ya michuano hiyo iliyoingia msimu wa tatu tangu iliporejeshwa rasmi?

More Stories

Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
28m ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
29m ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
1h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
2h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
9h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
14h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
14h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
16h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
16h ago
READ MORE β†’