Local,Normal News,Yanga, Simba

EFM yaiangukia Yanga, Oruma agoma kuomba radhi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Apr 2026
EFM yaiangukia Yanga, Oruma agoma kuomba radhi

Sakata kati ya klabu ya Yanga na vyombo vya habari vya EFM na TVE limechukua sura mpya kufuatia maudhui yaliyorushwa Aprili 17, 2026 kwenye kipindi cha michezo cha Namba 10. Maudhui hayo, yaliyotolewa na mchambuzi Wilson Oruma maarufu kama >Mzee wa Jambia, yameibua mjadala mkubwa miongoni mwa wadau wa soka nchini.

Akizungumza na wanahabari, Mkuu wa Idara ya Michezo wa EFM na TVE, Abbisay Stephen Jr, alieleza kuwa Aprili 20 walipokea barua kutoka kwa Mwanasheria wa klabu ya Yanga. Barua hiyo ilieleza kusudio la kuchukua hatua za kisheria dhidi ya taasisi hiyo kwa madai ya kashfa na uchochezi uliodaiwa kufanywa kupitia kauli za mchambuzi huyo.

Abbisay alisisitiza kuwa EFM na TVE hazina utaratibu wa kurusha maudhui chonganishi au yasiyo na mizania ya ushahidi. Alifafanua kuwa kauli zote zilizotolewa na Oruma zilikuwa ni maoni yake binafsi na si msimamo rasmi wa kituo hicho.

β€œNi kosa kutumia jukwaa letu kinyume na taratibu zinazofahamika. Tayari tumeshachukua hatua mbalimbali, ikiwemo kufuta maudhui yote husika na kumtaka mhusika kuomba radhi kupitia majukwaa yetu,” alisema Abbisay.

Hata hivyo, jitihada za kumtaka Oruma aombe radhi zimegonga mwamba, baada ya mchambuzi huyo kugoma kufanya hivyo. Kwa mujibu wa Abbisay, Oruma amesimama kidete akieleza kuwa yuko tayari kwenda mahakamani kujitetea.

Uamuzi huo umeongeza mvutano katika sakata hilo, huku klabu ya Yanga tayari ikithibitisha kufungua shauri mahakamani dhidi ya mchambuzi huyo. Hatua hii inaashiria kuwa mgogoro huo sasa umeingia katika hatua ya kisheria, na hatima yake huenda ikaamuliwa na vyombo vya sheria.

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
3h ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
5h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
7h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
7h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
8h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
8h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
9h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
17h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
21h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
21h ago
READ MORE β†’