EFM yaiangukia Yanga, Oruma agoma kuomba radhi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd April 2026


EFM yaiangukia Yanga, Oruma agoma kuomba radhi

Sakata kati ya klabu ya Yanga na vyombo vya habari vya EFM na TVE limechukua sura mpya kufuatia maudhui yaliyorushwa Aprili 17, 2026 kwenye kipindi cha michezo cha Namba 10. Maudhui hayo, yaliyotolewa na mchambuzi Wilson Oruma maarufu kama >Mzee wa Jambia, yameibua mjadala mkubwa miongoni mwa wadau wa soka nchini.

Akizungumza na wanahabari, Mkuu wa Idara ya Michezo wa EFM na TVE, Abbisay Stephen Jr, alieleza kuwa Aprili 20 walipokea barua kutoka kwa Mwanasheria wa klabu ya Yanga. Barua hiyo ilieleza kusudio la kuchukua hatua za kisheria dhidi ya taasisi hiyo kwa madai ya kashfa na uchochezi uliodaiwa kufanywa kupitia kauli za mchambuzi huyo.

Abbisay alisisitiza kuwa EFM na TVE hazina utaratibu wa kurusha maudhui chonganishi au yasiyo na mizania ya ushahidi. Alifafanua kuwa kauli zote zilizotolewa na Oruma zilikuwa ni maoni yake binafsi na si msimamo rasmi wa kituo hicho.

β€œNi kosa kutumia jukwaa letu kinyume na taratibu zinazofahamika. Tayari tumeshachukua hatua mbalimbali, ikiwemo kufuta maudhui yote husika na kumtaka mhusika kuomba radhi kupitia majukwaa yetu,” alisema Abbisay.

Hata hivyo, jitihada za kumtaka Oruma aombe radhi zimegonga mwamba, baada ya mchambuzi huyo kugoma kufanya hivyo. Kwa mujibu wa Abbisay, Oruma amesimama kidete akieleza kuwa yuko tayari kwenda mahakamani kujitetea.

Uamuzi huo umeongeza mvutano katika sakata hilo, huku klabu ya Yanga tayari ikithibitisha kufungua shauri mahakamani dhidi ya mchambuzi huyo. Hatua hii inaashiria kuwa mgogoro huo sasa umeingia katika hatua ya kisheria, na hatima yake huenda ikaamuliwa na vyombo vya sheria.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’