Local,Normal News,Azam, Yanga

Ibenge aipania Yanga nusu fainali Muungano Cup

Joel JJ By Joel JJ
24 Apr 2026
Ibenge aipania Yanga nusu fainali Muungano Cup

Kocha Mkuu wa Azam Fc Florent Ibenge amesema kikosi chake kitakuwa tayari kwa mchezo wa nusu fainali kombe la Muungano dhidi ya Yanga ambao utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa New Amaan Complex.

Azam Fc walitinga nusu fanali ya michuano hiyo baada ya kuichapa KVZ mabao 2-0 huku Yanga ambao ni mabingwa watetezi, wakiichapa Muembe Makumbi mabao 4-0 kwenye mchezo wa robo fainali.

Ibenge ametamba kuwa kikosi chake kitakuwa tayari kukabiliana na timu bora zaidi Tanzania Bara (Yanga) wakitoka kuiondosha mashindanoni timu bora visiwani Zanzibar (KVZ)

“Ni kweli tunakwenda kukutana na Yanga, utakuwa mchezo mgumu lakini sisi Azam hizo ndio mechi ambazo wakati wote tunapenda kuzicheza, tutajiandaa sawasawa kukutana nao"

“Mechi za namna hii zinakuimarisha na kujua ubora wa timu yako, tumetoka kuitoa timu bora ya hapa Zanzibar, haikuwa rahisi lakini tutakwenda kukutana tena na timu bora ya Ligi ya Bara,” alisema.

Hii itakuwa mechi ya tatu kwa Azam Fc kukutana na Yanga mwaka huu ikiwa ni ya pili timu hizo kukutana visiwani Zanzibar.

Yanga ilitwaa taji la Mapinduzi mwezi Januari baada ya kuifunga Azam Fc kwa mikwaju ya penati baada ya suluhu ya bila kufungana.

Timu hizo pia zimekutana kwenye mchezo wa ligi kuu ambao pia ulimalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →