Ibenge aipania Yanga nusu fainali Muungano Cup

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th April 2026


Ibenge aipania Yanga nusu fainali Muungano Cup

Kocha Mkuu wa Azam Fc Florent Ibenge amesema kikosi chake kitakuwa tayari kwa mchezo wa nusu fainali kombe la Muungano dhidi ya Yanga ambao utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa New Amaan Complex.

Azam Fc walitinga nusu fanali ya michuano hiyo baada ya kuichapa KVZ mabao 2-0 huku Yanga ambao ni mabingwa watetezi, wakiichapa Muembe Makumbi mabao 4-0 kwenye mchezo wa robo fainali.

Ibenge ametamba kuwa kikosi chake kitakuwa tayari kukabiliana na timu bora zaidi Tanzania Bara (Yanga) wakitoka kuiondosha mashindanoni timu bora visiwani Zanzibar (KVZ)

β€œNi kweli tunakwenda kukutana na Yanga, utakuwa mchezo mgumu lakini sisi Azam hizo ndio mechi ambazo wakati wote tunapenda kuzicheza, tutajiandaa sawasawa kukutana nao"

β€œMechi za namna hii zinakuimarisha na kujua ubora wa timu yako, tumetoka kuitoa timu bora ya hapa Zanzibar, haikuwa rahisi lakini tutakwenda kukutana tena na timu bora ya Ligi ya Bara,” alisema.

Hii itakuwa mechi ya tatu kwa Azam Fc kukutana na Yanga mwaka huu ikiwa ni ya pili timu hizo kukutana visiwani Zanzibar.

Yanga ilitwaa taji la Mapinduzi mwezi Januari baada ya kuifunga Azam Fc kwa mikwaju ya penati baada ya suluhu ya bila kufungana.

Timu hizo pia zimekutana kwenye mchezo wa ligi kuu ambao pia ulimalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’