Kocha Yanga atarajia nusu fainali ngumu dhidi ya Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th April 2026


Kocha Yanga atarajia nusu fainali ngumu dhidi ya Azam Fc

Kocha Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, amesema kikosi chake kiko tayari kwa mtanange mgumu wa nusu fainali ya Kombe la Muungano dhidi ya Azam FC utakaopigwa Jumamosi katika Uwanja wa New Amaan Complex.

Akizungumza na waandishi wa habari visiwani Zanzibar, Goncalves alisema licha ya muda mfupi wa maandalizi, kikosi chake kimejiandaa vyema kwa ajili ya mchezo huo muhimu, akisisitiza kuwa wanatarajia ushindani mkali.

Alisema Azam FC ni miongoni mwa timu bora na imekuwa ikipeleka upinzani mkubwa kila wanapokutana, hali inayoongeza uzito wa pambano hilo.

β€œTunatarajia kuwa na mchezo mgumu na wa ushindani mkubwa kwa sababu tunakutana na timu yenye ubora. Kila mara tunapocheza na Azam FC huwa wanatupa upinzani mkali,” alisema Goncalves.

Aliongeza kuwa pamoja na ratiba kuwa ngumu kutokana na ukaribu wa mechi kwenye michuano hiyo pamoja na ligi, kikosi chake kimefanya maandalizi kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha kinafikia malengo ya kutinga fainali.

Yanga, ambao ni mabingwa watetezi wa michuano hiyo, wanalisaka taji hilo kwa msimu wa pili mfululizo, ushindi utawathibitishia kuandikisha fainali yao ya pili mtawalia.

Mshindi wa mchezo huo atasonga mbele kusubiri mshindi wa nusu fainali nyingine kati ya Mlandege FC na Simba SC, ambao watakutana Jumapili.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’