Local,Normal News,Yanga, Azam

Kocha Yanga atarajia nusu fainali ngumu dhidi ya Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
24 Apr 2026
Kocha Yanga atarajia nusu fainali ngumu dhidi ya Azam Fc

Kocha Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, amesema kikosi chake kiko tayari kwa mtanange mgumu wa nusu fainali ya Kombe la Muungano dhidi ya Azam FC utakaopigwa Jumamosi katika Uwanja wa New Amaan Complex.

Akizungumza na waandishi wa habari visiwani Zanzibar, Goncalves alisema licha ya muda mfupi wa maandalizi, kikosi chake kimejiandaa vyema kwa ajili ya mchezo huo muhimu, akisisitiza kuwa wanatarajia ushindani mkali.

Alisema Azam FC ni miongoni mwa timu bora na imekuwa ikipeleka upinzani mkubwa kila wanapokutana, hali inayoongeza uzito wa pambano hilo.

β€œTunatarajia kuwa na mchezo mgumu na wa ushindani mkubwa kwa sababu tunakutana na timu yenye ubora. Kila mara tunapocheza na Azam FC huwa wanatupa upinzani mkali,” alisema Goncalves.

Aliongeza kuwa pamoja na ratiba kuwa ngumu kutokana na ukaribu wa mechi kwenye michuano hiyo pamoja na ligi, kikosi chake kimefanya maandalizi kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha kinafikia malengo ya kutinga fainali.

Yanga, ambao ni mabingwa watetezi wa michuano hiyo, wanalisaka taji hilo kwa msimu wa pili mfululizo, ushindi utawathibitishia kuandikisha fainali yao ya pili mtawalia.

Mshindi wa mchezo huo atasonga mbele kusubiri mshindi wa nusu fainali nyingine kati ya Mlandege FC na Simba SC, ambao watakutana Jumapili.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
6h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
11h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
11h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
13h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
14h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
17h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
19h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
20h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’