Bajaber apewa nafasi ya kujipambania Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th April 2026


Bajaber apewa nafasi ya kujipambania Simba

Ni kama kiungo mshambuliaji wa Simba SC Mohamed Bajaber, amepewa nafasi ya kujitetea ili kurejea rasmi kikosini baada ya kukumbwa na mfululizo wa majeraha yaliyomuweka nje kwa muda mrefu.

Bajaber alirejea uwanjani jana baada ya kukosekana kwa muda mrefu, alipokuwa sehemu ya kikosi cha Simba kilichocheza robo fainali ya Kombe la Muungano dhidi ya Mafunzo FC. Katika mchezo huo, Simba ilitinga hatua ya nusu fainali baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Tangu ajiunge na Simba akitokea Polisi FC katika dirisha la usajili la Julai mwaka jana, mchezaji huyo hajapata nafasi ya kuonyesha kiwango chake kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara.

Majeraha hayo yamekuwa kikwazo kikubwa kwake pamoja na mashabiki wa Simba waliokuwa na matarajio ya kushuhudia uwezo wake uwanjani.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa Simba ulilazimika kumuondoa kwenye mfumo wa usajili katika dirisha dogo ili kutoa nafasi kwa mchezaji mwingine wa kigeni, huku ukimpa muda wa kuimarika kiafya.

Hata hivyo, Bajaber aliendelea kufanya mazoezi na kikosi hicho, jambo linaloashiria kuwa bado yupo kwenye mipango ya timu hiyo.

Kurejea kwake kupitia michuano ya Kombe la Muungano kunaonekana kuwa ni mwanzo wa juhudi zake za kujithibitisha upya ili kurejeshwa rasmi kikosini.

Bajaber bado ana mkataba wa muda mrefu na Simba, huenda Wekundu hao wa Msimbazi wakamrejesha kikosini kwenye dirisha lijalo la usajili kama watajiridhisha amepona sawa sawa na anaweza kutumika.

Lakini kama mambo yatakuwa tofauti huenda kwenye wakati mgumu zaidi kwani huenda mabosi wa Simba wasiwe na muda mrefu zaidi wa kumsubiri hasa ikizingatiwa ni mchezaji wa kigeni.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’