Local,Normal News,Simba

Bajaber apewa nafasi ya kujipambania Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
24 Apr 2026
Bajaber apewa nafasi ya kujipambania Simba

Ni kama kiungo mshambuliaji wa Simba SC Mohamed Bajaber, amepewa nafasi ya kujitetea ili kurejea rasmi kikosini baada ya kukumbwa na mfululizo wa majeraha yaliyomuweka nje kwa muda mrefu.

Bajaber alirejea uwanjani jana baada ya kukosekana kwa muda mrefu, alipokuwa sehemu ya kikosi cha Simba kilichocheza robo fainali ya Kombe la Muungano dhidi ya Mafunzo FC. Katika mchezo huo, Simba ilitinga hatua ya nusu fainali baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Tangu ajiunge na Simba akitokea Polisi FC katika dirisha la usajili la Julai mwaka jana, mchezaji huyo hajapata nafasi ya kuonyesha kiwango chake kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara.

Majeraha hayo yamekuwa kikwazo kikubwa kwake pamoja na mashabiki wa Simba waliokuwa na matarajio ya kushuhudia uwezo wake uwanjani.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa Simba ulilazimika kumuondoa kwenye mfumo wa usajili katika dirisha dogo ili kutoa nafasi kwa mchezaji mwingine wa kigeni, huku ukimpa muda wa kuimarika kiafya.

Hata hivyo, Bajaber aliendelea kufanya mazoezi na kikosi hicho, jambo linaloashiria kuwa bado yupo kwenye mipango ya timu hiyo.

Kurejea kwake kupitia michuano ya Kombe la Muungano kunaonekana kuwa ni mwanzo wa juhudi zake za kujithibitisha upya ili kurejeshwa rasmi kikosini.

Bajaber bado ana mkataba wa muda mrefu na Simba, huenda Wekundu hao wa Msimbazi wakamrejesha kikosini kwenye dirisha lijalo la usajili kama watajiridhisha amepona sawa sawa na anaweza kutumika.

Lakini kama mambo yatakuwa tofauti huenda kwenye wakati mgumu zaidi kwani huenda mabosi wa Simba wasiwe na muda mrefu zaidi wa kumsubiri hasa ikizingatiwa ni mchezaji wa kigeni.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
10h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
13h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
19h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’