Local,Transfer News,Pamba, Simba

Larry Bwalya sasa kukamilisha usajili wake Pamba Jiji

Joel JJ By Joel JJ
β€’
24 Apr 2026
Larry Bwalya sasa kukamilisha usajili wake Pamba Jiji

Kiungo fundi wa kimataifa wa Zambia ambaye amewahi kutamba na klabu ya Simba, Larry Bwalya, yuko hatua za mwisho kujiunga na Pamba Jiji baada ya pande zote mbili kufikia makubaliano ya kisheria kuhusu usajili wake.

Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa, mchakato wa awali wa usajili huo ulikwama kutokana na mkataba wake na klabu ya Napsa Stars ya nchini Zambia. Hata hivyo, sasa changamoto hiyo imepatiwa suluhu baada ya makubaliano kufikiwa kwa lengo la kumlinda mchezaji pamoja na maslahi ya klabu husika.

Bwalya anatarajiwa kujiunga rasmi na kikosi hicho cha mkoani Mwanza kuelekea msimu wa 2026/27, mara atakapomaliza mkataba wake wa sasa na klabu yake.

Taarifa zinaeleza kuwa Pamba Jiji tayari imeanza utekelezaji wa makubaliano hayo kwa kutoa sehemu ya ada ya usajili, huku kiasi kilichobaki kikitarajiwa kulipwa mara mchezaji huyo atakapowasili rasmi kuanza majukumu yake.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
4h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
9h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
11h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
11h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
15h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
17h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
18h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’