Real Madrid yazidi kupotea njia ubingwa La Liga

Joel JJ By Joel JJ ‱ 25th April 2026


Real Madrid yazidi kupotea njia ubingwa La Liga

Klabu ya Real Madrid imeendelea kupoteza mwelekeo katika mbio za ubingwa wa La Liga baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Real Betis, katika mchezo uliochezwa Ijumaa usiku.

Katika mchezo huo uliopigwa jijini Sevilla, Madrid walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia nyota wao VinĂ­cius JĂșnior aliyefunga mapema dakika ya 17, akimalizia vizuri shambulizi lililoanzishwa na Federico Valverde.

Hata hivyo, pamoja na kutengeneza nafasi kadhaa za kufunga mabao zaidi zikiwemo juhudi za Jude Bellingham na Kylian Mbappé, Madrid walishindwa kuongeza bao la pili, jambo lililowapa nafasi wapinzani wao kurejea mchezoni.

Dakika za lala salama, beki wa Betis Héctor Bellerín aliisawazishia timu yake bao muhimu dakika ya 93, akitumia uzembe wa safu ya ulinzi ya Madrid.

Matokeo hayo yamekuwa pigo kubwa kwa Real Madrid katika mbio za ubingwa, kwani sasa wanabaki nyuma kwa alama nane dhidi ya vinara wa ligi, huku wapinzani wao wakubwa FC Barcelona wakiwa na mchezo mkononi, hali inayoweza kuongeza pengo hilo hadi alama 11.

Kwa mujibu wa wachambuzi wa soka, sare hiyo imeifanya safari ya Madrid kuelekea ubingwa kuwa ngumu zaidi, huku presha sasa ikielekezwa kwenye mchezo ujao mkubwa wa El ClĂĄsico, ambao unaweza kuamua hatma ya mbio hizo.

Kwa upande wa Real Betis, matokeo hayo ni mafanikio makubwa dhidi ya timu yenye hadhi ya juu kama Madrid, huku wao wakiendelea kupambania nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →