Local,Normal News,Simba, Mlandege

Kocha Simba aipigia hesabu kali Mlandege Fc, Nusu Fainali Muungano Cup

Joel JJ By Joel JJ
25 Apr 2026
Kocha Simba aipigia hesabu kali Mlandege Fc, Nusu Fainali Muungano Cup

Kikosi cha Simba SC kimepania kufuzu hatua ya fainali ya Kombe la Muungano baada ya kocha mkuu Steve Barker kueleza wazi kuwa lengo lao ni kupata ushindi dhidi ya Mlandege FC katika mchezo wa nusu fainali utakaopigwa kesho Jumapili kwenye Uwanja wa New Amaan Complex visiwani Zanzibar.

Simba inatarajiwa kushuka dimbani huku ikiingia kwenye mchezo huo ikijua wazi haitakuwa kazi rahisi kutokana na ubora na historia ya wapinzani wao, Mlandege FC ambao ni moja ya timu zenye ushawishi mkubwa visiwani humo.

Akizungumza na wanahabari mapema leo, Kocha Steve Barker alisisitiza kuwa maandalizi ya timu yake yamekamilika na wachezaji wako tayari kupambana kuhakikisha wanapata matokeo chanya.

“Maandalizi ya mchezo huu yamekamilika, wachezaji wangu wako tayari kwenda kufanya kile kilicho bora,” alisema Barker.

Aidha, alikiri kuwa wanakutana na timu ngumu na yenye mafanikio Zanzibar, jambo linaloifanya mechi hiyo kuwa ya ushindani mkubwa zaidi.

“Tunafahamu haitakuwa mechi rahisi kwa sababu tunakwenda kucheza dhidi ya timu yenye mafanikio zaidi hapa Zanzibar,” aliongeza kocha huyo.

Hata hivyo, Barker alibainisha kuwa Simba haijapunguza malengo yake na ina imani kubwa ya kuvuka hatua hiyo muhimu.

“Lakini tuko tayari na tuna matumaini makubwa ya kupata ushindi na kusonga mbele hatua ya fainali,” alisisitiza.

Mlandege FC, ikiwa timu pekee kutoka visiwani Zanzibar iliyofanikiwa kufika hatua ya nusu fainali, inatarajiwa kupata sapoti kubwa ya mashabiki wake, jambo linaloweza kuongeza presha kwa Simba SC katika mchezo huo muhimu.

Endapo Simba itafanikiwa kushinda, itakutana na mshindi wa mchezo mwingine wa nusu fainali kati ya Azam FC na Yanga SC, ambao unatarajiwa kupigwa leo.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
5h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
10h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
10h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
12h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
13h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
16h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
18h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
19h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →