Spurs yapata ushindi wa kwanza EPL 2026

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th April 2026


Spurs yapata ushindi wa kwanza EPL 2026

Klabu ya Tottenham Hotspur imepata ushindi wake wa kwanza mwaka 2026 katika Premier League baada ya kuichapa Wolverhampton Wanderers bao 1-0 katika mchezo uliochezwa Jumamosi.

Bao pekee la mchezo huo lililofungwa na Palhinha lilitosha kuwapa Spurs pointi tatu muhimu, wakikatiza mfululizo wa matokeo mabaya uliokuwa umeiweka timu hiyo katika hatari kubwa ya kushuka daraja.

Licha ya ushindi huo, Tottenham bado inasalia katika nafasi ya 18 alama mbili nyuma ya West Ham kwenye msimamo wa ligi, ikihitaji matokeo mazuri zaidi katika michezo iliyobaki ili kujinusuru.

Katika mchezo mwingine, West Ham United iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Everton, katika pambano lililokuwa na ushindani mkali.

West Ham ilianza vyema kwa kupata bao la kuongoza kabla ya Everton kusawazisha, lakini bao la dakika za mwisho liliihakikishia ushindi huo muhimu wenyeji hao. Matokeo hayo yameiongezea West Ham matumaini ya kubaki ligi kuu, huku ikijinasua kidogo kutoka eneo la kushuka daraja.

Matokeo ya mechi nyingine, Fulham imeichapa Aston Villa bao 1-0 wakati Liverpool ikipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’