Klabu ya Tottenham Hotspur imepata ushindi wake wa kwanza mwaka 2026 katika Premier League baada ya kuichapa Wolverhampton Wanderers bao 1-0 katika mchezo uliochezwa Jumamosi.
Bao pekee la mchezo huo lililofungwa na Palhinha lilitosha kuwapa Spurs pointi tatu muhimu, wakikatiza mfululizo wa matokeo mabaya uliokuwa umeiweka timu hiyo katika hatari kubwa ya kushuka daraja.





