International,Normal News,Tottenham, Wolves, West Ham, Everton, Liverpool, Crystal

Spurs yapata ushindi wa kwanza EPL 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
25 Apr 2026
Spurs yapata ushindi wa kwanza EPL 2026

Klabu ya Tottenham Hotspur imepata ushindi wake wa kwanza mwaka 2026 katika Premier League baada ya kuichapa Wolverhampton Wanderers bao 1-0 katika mchezo uliochezwa Jumamosi.

Bao pekee la mchezo huo lililofungwa na Palhinha lilitosha kuwapa Spurs pointi tatu muhimu, wakikatiza mfululizo wa matokeo mabaya uliokuwa umeiweka timu hiyo katika hatari kubwa ya kushuka daraja.

Licha ya ushindi huo, Tottenham bado inasalia katika nafasi ya 18 alama mbili nyuma ya West Ham kwenye msimamo wa ligi, ikihitaji matokeo mazuri zaidi katika michezo iliyobaki ili kujinusuru.

Katika mchezo mwingine, West Ham United iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Everton, katika pambano lililokuwa na ushindani mkali.

West Ham ilianza vyema kwa kupata bao la kuongoza kabla ya Everton kusawazisha, lakini bao la dakika za mwisho liliihakikishia ushindi huo muhimu wenyeji hao. Matokeo hayo yameiongezea West Ham matumaini ya kubaki ligi kuu, huku ikijinasua kidogo kutoka eneo la kushuka daraja.

Matokeo ya mechi nyingine, Fulham imeichapa Aston Villa bao 1-0 wakati Liverpool ikipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
7h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’