Local,Normal News,Yanga

Luvanga anaiwakilisha vyema Tanzania soka la Wanawake Saudia

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Apr 2026
Luvanga anaiwakilisha vyema Tanzania soka la Wanawake Saudia

Nyota wa soka la wanawake kutoka Tanzania, Clara Luvanga, ameendelea kuandika historia nchini Saudi Arabia baada ya kuweka rekodi ya kipekee katika Saudi Women's Premier League, akionyesha ubora mkubwa.

Mshambuliaji huyo wa Al-Nassr Women amemaliza msimu wa 2025/26 akiwa mfungaji bora wa ligi hiyo kwa mabao 24, idadi ambayo si tu imempa tuzo ya ufungaji bora bali pia kuvunja rekodi yake mwenyewe ya misimu iliyopita.

Huu ni muendelezo wa kiwango cha juu kwa Luvanga ambaye katika misimu mitatu mfululizo ameonyesha kupanda kwa kasi ya kufunga mabao akianza na mabao 11, kisha 21 na sasa 24, rekodi inayodhihirisha ukuaji mkubwa wa kiwango chake.

Safari ya rekodi na ubora wake

Luvanga si mchezaji wa kawaida. Tangu ajiunge na Al-Nassr mwaka 2023, amekuwa tegemeo kubwa la safu ya ushambuliaji, akisaidia timu hiyo kutawala soka la wanawake nchini humo na hata kutwaa ubingwa wa ligi mara kadhaa.

Katika msimu huu pekee, mbali na mabao 24, Luvanga pia ameendelea kuwa tishio kwa mabeki, akifunga hat-trick kadhaa na kuiongoza timu yake kutwaa ubingwa mwingine wa ligi hiyo ambayo imeanzishwa hivi karibuni lakini inakua kwa kasi kubwa.

Kutoka Tanzania hadi kuwa nyota wa kimataifa

Akiwa na umri mdogo, Luvanga tayari ameweka jina lake kwenye ramani ya soka la dunia. Alianzia soka lake katika timu za ndani kabla ya kusajiliwa na Yanga Princeess ambayo ilimtambulisha zaidi na hatimaye kupata nafasi ya kucheza Ulaya na baadaye kuhamia Saudi Arabia ambako ameibuka kuwa mmoja wa washambuliaji hatari zaidi.

Uwezo wake wa kufunga, kasi na utulivu mbele ya lango vimemfanya kuwa mchezaji muhimu si tu kwa klabu yake bali pia kwa timu ya taifa ya Tanzania (Twiga Stars).

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’