Local,Normal News,Yanga, Simba

Goncalves atamba, ni fainali ya burudani kwa mashabiki

Joel JJ By Joel JJ
28 Apr 2026
Goncalves atamba, ni fainali ya burudani kwa mashabiki

Kocha mkuu wa Yanga, Rui Pedro Gonçalves, ameweka wazi kuwa kikosi chake kiko tayari kikamilifu kwa fainali ya Kombe la Muungano dhidi ya Simba SC, huku akisisitiza kuwa mchezo huo hautakuwa wa ushindani pekee bali pia burudani kwa mashabiki.

Mchezo huo mkubwa unatarajiwa kupigwa kesho Jumatano, Aprili 29 katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar, ukiwakutanisha wapinzani wakubwa wa soka la Tanzania.

Malengo ni kushinda kila mchezo

Akizungumza na wanahabari kabla ya fainali hiyo, Goncalves amesema Yanga imejipanga kushinda kila mchezo bila kujali ukubwa wa mashindano, huku akisisitiza kuwa nidhamu na malengo ya klabu ndiyo msingi wa mafanikio yao.

“Tulipoanza msimu tuliweka malengo yetu. Ukiachilia mbali mashindano yaliyopewa kipaumbele, msimamo wetu ni kushinda kila mechi,” alisema Goncalves.

Kocha huyo ameongeza kuwa kazi yake kubwa ni kuhakikisha wachezaji wanabaki katika kiwango bora na kuendelea kujiamini katika kila mchezo wanaocheza.

Burudani kwa mashabiki

Goncalves amesisitiza kuwa Yanga haitakwenda uwanjani kwa ajili ya ushindi pekee, bali pia kutoa burudani kwa mashabiki watakaojitokeza kwa wingi kushuhudia fainali hiyo.

“Wachezaji wangu wamejiandaa sio tu kucheza fainali, bali kutoa burudani. Tutakwenda kuburudisha mashabiki na sio tu kucheza,” alifafanua.

Ameongeza kuwa ana matarajio makubwa kutoka kwa kikosi chake, akiamini kuwa mchezo huo utakuwa wa kuvutia na wenye ushindani wa hali ya juu.

Zanzibar ni nyumbani kwa Yanga

Kocha huyo pia aligusia mapokezi mazuri ambayo timu yake imekuwa ikipata kila wanaposafiri sehemu mbalimbali nchini, akisisitiza kuwa Yanga inahisi kama ipo nyumbani popote Tanzania.

“Yanga inapokuwa ndani ya Tanzania Bara au visiwani ipo nyumbani. Tumepata mapokezi mazuri kila sehemu. Hapa Zanzibar tupo nyumbani,” alisema.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
4h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
9h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
11h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
11h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
15h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
17h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
18h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →