Baraza la FIFA limepitisha mabadiliko muhimu ya sheria yatakayotumika katika FIFA World Cup 2026, yakilenga kubadilisha mwenendo wa mchezo na kuongeza nidhamu kwa wachezaji wote, kuanzia nyota wakubwa hadi wale wa benchi. Hatua hii inaashiria mwanzo wa enzi mpya ya usimamizi wa soka katika mashindano hayo yatakayofanyika katika United States, Canada na Mexico.





