Rupia ajiweka pembeni Singida BS, sababu yatajwa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st May 2026


Rupia ajiweka pembeni Singida BS, sababu yatajwa

Mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya, Elvis Rupia, ameondoka katika klabu ya Singida Black Stars (Singida BS) aliyokuwa akiitumikia, kufuatia mgogoro unaodaiwa kuhusiana na malipo ya fedha za usajili.

Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na mchezaji huyo, Rupia amekuwa na mvutano na uongozi wa klabu hiyo kutokana na madai ya kutolipwa stahiki zake, hali iliyopelekea kufikia uamuzi wa kuondoka.

Inaelezwa kuwa hadi sasa hakuna mwafaka uliopatikana kati ya pande hizo mbili, jambo linalotia shaka uwezekano wa mshambuliaji huyo kurejea kikosini kabla ya msimu huu kumalizika.

Rupia, ambaye ni miongoni mwa washambuliaji wenye uzoefu katika ukanda wa Afrika Mashariki, ameichezea Singida BS kwa kipindi cha misimu mitatu, akitoa mchango wake katika safu ya ushambuliaji ya timu hiyo.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’