Yanga yafanya maandalizi Zanzibar, tayari kuikabili Simba Jumapili

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st May 2026


Yanga yafanya maandalizi Zanzibar, tayari kuikabili Simba Jumapili

Wakati watani zao Simba wakirejea jijini Dar es salaam jana baada ya kutwaa kombe la Muungano, kikosi cha Yanga kilisalia visiwani Zanzibar kujiandaa na mchezo wa ligi kuu utakaowakutanisha na Simba kwa mara ya pili katika kipindi cha siku tano.

Jumapili May 03 timu hizo zitachuana tena katika mchezo wa ligi kuu ambao matokeo yake huenda yakawa na maamuzi kwenye mbio za ubingwa msimu huu.

Yanga chini ya kocha Pedro Goncalves imepania kulipa kisasi dhidi ya kipigo kutoka kwa watani zao Simba na kumaliza mfululizo wa mechi 7 za bila ushindi kwa Simba.

Meneja wa Yanga Walter Harrison amesema wanaendelea na maandalizi yao kuelekea mchezo huku akibainisha kuwa wachezaji wao wote wako katika hali nzuri, hakuna changamoto za majeruhi wapya baada ya fainali ya komb la Muungano.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’