Local,Normal News,Simba, Yanga

Ahmed afunguka hatma ya Oura, Kibabage, Kagoma dabi ya Jumapili

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 May 2026
Ahmed afunguka hatma ya Oura, Kibabage, Kagoma dabi ya Jumapili

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba SC Ahmed Ally, ametoa taarifa nzuri kwa mashabiki wa timu hiyo kuhusu hali ya majeruhi wake kuelekea mchezo mkubwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Young Africans SC, maarufu kama dabi ya Kariakoo.

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Jumapili, Mei 03, katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, ukiwa ni moja ya mechi zinazovuta hisia kubwa zaidi katika soka la Tanzania.

Wote wako fiti kwa dabi

Ahmed Ally amethibitisha kuwa nyota watatu muhimu wa kikosi hicho, Anicet Oura, Nickson Kibabage na Yusuph Kagoma wote wamepona majeraha waliyoyapata katika mchezo uliopita wa fainali ya Kombe la Muungano na sasa wako tayari kuanza mazoezi pamoja na kikosi.

Wachezaji hao walishindwa kumaliza mchezo huo kutokana na matatizo ya majeraha, hali iliyoibua hofu kwa mashabiki wa Simba kuhusu uwezekano wao kukosa dabi hiyo muhimu.

Kauli ya Ahmed Ally

Akizungumza kuhusu hali ya kikosi, Ahmed Ally alisema:

"Napenda kuwajulisha kwamba wachezaji wote (Oura, Kibabage na Kagoma) ambao walitolewa katika mchezo wa fainali ya Kombe la Muungano kwa kuumia, wote wako tayari kwa mchezo wa Jumapili. Ninapozungumza hapa wachezaji wapo vizuri kabisa. Cha kufanya ni kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kulinda hali zao."

Simba kuingia kambini

Simba SC iliingia kambini rasmi jana kuanza maandalizi ya mwisho ya mchezo huo muhimu dhidi ya watani wao wa jadi. Timu hiyo inaendelea kujifua kwa kasi kubwa ikiwa na lengo la kuhakikisha inapata matokeo chanya katika moja ya michezo migumu zaidi ya msimu.

Dabi hiyo ya Kariakoo inatarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku pande zote mbili zikihitaji ushindi kwa malengo tofauti ya msimamo wa ligi.

Simba inahitaji ushindi ili kupunguza gap la pointi dhidi ya watani zao Yanga kuwa 2 ili kusalia katika vita ya kuwania ubingwa.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’