Ceballos katika mvutano na Arbeloa Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ • 2nd May 2026


Ceballos katika mvutano na Arbeloa Real Madrid

Mgogoro mkubwa umeibuka ndani ya klabu ya Real Madrid baada ya kiungo Dani Ceballos kuingia kwenye mvutano mkali na kocha Álvaro Arbeloa, hali iliyofikia hatua ya kuvunjika kabisa kwa uhusiano wao.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka gazeti la Marca, Ceballos hataitwa tena kwenye kikosi cha mechi hadi mwisho wa msimu, huku Arbeloa akidaiwa “hataki hata kumuona” mchezaji huyo.

Tukio hilo linafuatia kikao cha ana kwa ana kilichofanyika mazoezini Valdebebas, ambapo mazungumzo yaligeuka kuwa mabaya na kuashiria mwisho wa uhusiano wao .

Inaelezwa kuwa baada ya kikao hicho, Ceballos aliwaambia wachezaji wenzake wazi kuwa hataki tena kuwa na mawasiliano yoyote na kocha wake, kauli iliyothibitisha kuwa mgogoro huo umefikia hatua ya “hakuna kurudi nyuma” .

Hali hiyo imeathiri moja kwa moja nafasi yake uwanjani. Licha ya kuwa fiti, kiungo huyo amekuwa akiachwa nje ya kikosi katika mechi muhimu za La Liga, jambo lililozua maswali mengi kwa mashabiki.

Ndani ya klabu, uongozi unaonekana kusimama upande wa kocha, ukiuchukulia uamuzi huo kama wa kiufundi, lakini ukweli ni kwamba uhusiano wao umevunjika kabisa .

Kwa sasa, ishara zote zinaonyesha kuwa huu ndio mwisho wa safari ya Ceballos katika Santiago Bernabéu. Licha ya kuwa na mkataba unaoendelea hadi 2027, mipango iliyopo ni wazi, ataondoka majira ya kiangazi kutafuta changamoto mpya, huku klabu ya zamani ya Real Betis ikitajwa kama moja ya chaguo lake kuu .


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →