International,Normal News,Real Madrid, Arsenal, Betis

Ceballos katika mvutano na Arbeloa Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ
2 May 2026
Ceballos katika mvutano na Arbeloa Real Madrid

Mgogoro mkubwa umeibuka ndani ya klabu ya Real Madrid baada ya kiungo Dani Ceballos kuingia kwenye mvutano mkali na kocha Álvaro Arbeloa, hali iliyofikia hatua ya kuvunjika kabisa kwa uhusiano wao.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka gazeti la Marca, Ceballos hataitwa tena kwenye kikosi cha mechi hadi mwisho wa msimu, huku Arbeloa akidaiwa “hataki hata kumuona” mchezaji huyo.

Tukio hilo linafuatia kikao cha ana kwa ana kilichofanyika mazoezini Valdebebas, ambapo mazungumzo yaligeuka kuwa mabaya na kuashiria mwisho wa uhusiano wao .

Inaelezwa kuwa baada ya kikao hicho, Ceballos aliwaambia wachezaji wenzake wazi kuwa hataki tena kuwa na mawasiliano yoyote na kocha wake, kauli iliyothibitisha kuwa mgogoro huo umefikia hatua ya “hakuna kurudi nyuma” .

Hali hiyo imeathiri moja kwa moja nafasi yake uwanjani. Licha ya kuwa fiti, kiungo huyo amekuwa akiachwa nje ya kikosi katika mechi muhimu za La Liga, jambo lililozua maswali mengi kwa mashabiki.

Ndani ya klabu, uongozi unaonekana kusimama upande wa kocha, ukiuchukulia uamuzi huo kama wa kiufundi, lakini ukweli ni kwamba uhusiano wao umevunjika kabisa .

Kwa sasa, ishara zote zinaonyesha kuwa huu ndio mwisho wa safari ya Ceballos katika Santiago Bernabéu. Licha ya kuwa na mkataba unaoendelea hadi 2027, mipango iliyopo ni wazi, ataondoka majira ya kiangazi kutafuta changamoto mpya, huku klabu ya zamani ya Real Betis ikitajwa kama moja ya chaguo lake kuu .

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
31m ago
READ MORE →
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
2h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
4h ago
READ MORE →
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
4h ago
READ MORE →
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
5h ago
READ MORE →
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
6h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
13h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
18h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
18h ago
READ MORE →