Leo jijini Dar es Salaam, macho na masikio ya mashabiki wa soka yanaelekezwa kwenye dimba la Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni, ambapo patapigwa mtanange mkubwa wa Ligi Kuu ya NBC kati ya watani wa jadi, Simba SC dhidi ya Yanga SC.
Ni mchezo unaokuja ukiwa na uzito mkubwa kwenye mbio za ubingwa msimu huu, huku kila upande ukiingia uwanjani ukiwa na hesabu zake.



