Local,Normal News,Mashujaa, Mbeya, Prisons, TRA

Mashujaa yaiduwaza TRA United wakati Mbeya City ikishinda Mbeya Derby

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 May 2026
Mashujaa yaiduwaza TRA United wakati Mbeya City ikishinda Mbeya Derby

Ligi Kuu NBC imeendelea leo kwa michezo miwili kupigw katika miji ya Kigoma na Mbeya.

Mashujaa FC waibuka na ushindi Kigoma

Katika Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma, Mashujaa FC waliibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya TRA United.

Bao pekee la mchezo lilifungwa na Ismail Mgunda dakika ya 37, bao lililodumu hadi mwisho wa dakika 90. Ushindi huo unaipa Mashujaa alama muhimu katika harakati zao za kupanda juu ya msimamo wa ligi.

TRA United walijaribu kusawazisha katika kipindi cha pili lakini walishindwa kupenya safu ya ulinzi ya Mashujaa iliyokuwa imara.

Mbeya Derby: Mbeya City yaibuka kidedea

Katika dabi ya jiji la Mbeya, uwanja wa Sokoine, Mbeya City waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo uliokuwa na presha kubwa kwa pande zote.

Mbeya City walianza vyema kwa kupata bao la kuongoza kupitia Eliud Ambokile dakika ya 19. Hata hivyo, Tanzania Prisons walirejea mchezoni baada ya Emmanuel Martin kusawazisha dakika ya 33.

Katika kipindi cha pili, presha ya Mbeya City ilizaa matunda baada ya beki wa Prisons, Martin Mhilu, kujifunga na kuipa Mbeya City bao la ushindi.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’