International,Normal News,Chelsea, Nottinhham Forest, Local

Chelsea labda wachapwe viboko wataamka usingizini

Joel JJ By Joel JJ
4 May 2026
Chelsea labda wachapwe viboko wataamka usingizini

Klabu ya Chelsea imeendelea kuporomoka kwenye Premier League baada ya kuchapwa mabao 3-1 na Nottingham Forest katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la Stamford Bridge.

Mshambuliaji wa Forest, Taiwo Awoniyi, alikuwa nyota wa mchezo huo baada ya kufunga mabao mawili ya mapema na kuwapa wageni mwanzo mzuri. Awoniyi alifungua pazia la mabao dakika ya 2 kabla ya kurejea tena kufunga bao la tatu dakika ya 52.

Bao jingine la Nottingham Forest lilifungwa na Igor Jesus kwa njia ya mkwaju wa penalti dakika ya 15, baada ya safu ya ulinzi ya Chelsea kufanya makosa yaliyoigharimu timu hiyo.

Chelsea walipata bao lao pekee mwishoni mwa mchezo kupitia João Pedro, lakini halikutosha kuokoa jahazi lao lililokuwa tayari limezama.

Licha ya kupata nafasi kadhaa, ikiwemo penalti, Chelsea walishindwa kuitumia ipasavyo, jambo lililozidi kuongeza presha kwa benchi la ufundi na wachezaji wake.

Matokeo hayo yanaifanya Chelsea kuendelea kuyumba katika msimamo wa ligi, huku Nottingham Forest wakijiongezea matumaini ya kubaki salama katika ligi hiyo baada ya ushindi muhimu ugenini.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →