International,Normal News,Athletic Club, Borussia Dortmund, LaLiga

Edin Terzic atangazwa kuwa kocha mpya wa Bilbao.

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
β€’
5 May 2026
Edin Terzic atangazwa kuwa kocha mpya wa Bilbao.

Klabu ya Athletic Club imemtangaza rasmi Edin Terzic kuwa kocha mkuu mpya, akichukua mikoba ya Ernesto Valverde. Terzic amesaini mkataba utakaomuweka klabuni hapo hadi june 2028, katika viunga vya dimba la san mames.

Kocha huyo raia wa ujerumani anajiunga na bilbao, ambapo aliwahi kuiongoza timu hiyo hadi kufika fainali ya UEFA Champions League. Uzoefu huo unampa hadhi ya kuaminiwa kuleta mabadiliko na ushindani mpya ndani ya kikosi cha Athletic club.

Kuondoka kwa Valverde kunatajwa kuchochewa na sababu kadhaa, ikiwemo matokeo yasiyoridhisha pamoja na ukosefu wa maendeleo ya wazi ya timu katika kipindi cha hivi karibuni. Uongozi wa klabu uliamua kufanya mabadiliko ili kurejesha ari ya ushindani wa timu na matarajio ya mashabiki wa Bilbao.

kwa upande wake, Terzic anatarajiwa kuleta mbinu za kisasa, uwezzo wa kuunganisha wachezaji na ari mpya ya ushindani. Akiwa anajulikana kwa uwezo wake wa kuhamasisha timu na kujenga mshikamano, macho yote sasa yako kwake kuona kama ataweza kuirejesha Athletic Clib katoka ubora wake unaotarajiwa.

kwa ujumla, uteuzi huu unaashiria mwanzo wa safari mpya kwa Bilbao, huku mashabiki wakisubiri kuona matokeo ya uongozi mpya chini ya terzic kutoka dortmund hadi Bilbao, changamoto mpya imeanza rasmi.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
6h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
11h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
11h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
13h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
14h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
17h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
19h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
20h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’