Local,Simba, Marumo, Transfer News

Simba yahusishwa na kiungo Marumo Gallants

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 May 2026
Simba yahusishwa na kiungo Marumo Gallants

Klabu ya Simba SC inatajwa kuingia kwenye mazungumzo ya kumuwania kiungo mkabaji Ibrahim Bance kutoka Marumo Gallants ya Afrika Kusini.

Kiungo huyo raia wa Burkina Faso anatajwa kuwa chaguo la kocha wa Simba, Steve Barker, ambaye anaamini ataongeza nguvu katika eneo la kiungo mkabaji ndani ya timu hiyo.

Barker anatafuta mbadala sahihi wa Allasane Kante, ambaye ameripotiwa huenda akapewa mkono wa kwaheri mwishoni mwa msimu.

Taarifa zinaeleza kuwa Bance anatarajiwa kumaliza mkataba wake na Marumo Gallants mwishoni mwa msimu huu, hali inayofungua mlango kwa Simba kumpata bila gharama kubwa akiwa kama mchezaji huru.

Iwapo mazungumzo hayo yatafanikiwa, basi Simba itakuwa imepata kiungo mwenye uwezo wa kukaba, kusoma mchezo na kusaidia ujenzi wa mashambulizi kutoka chini akishirikiana na viungo wengine.

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
5h ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
7h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
9h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
9h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
9h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
10h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
10h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
18h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
22h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
23h ago
READ MORE β†’