Simba yahusishwa na kiungo Marumo Gallants

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th May 2026


Simba yahusishwa na kiungo Marumo Gallants

Klabu ya Simba SC inatajwa kuingia kwenye mazungumzo ya kumuwania kiungo mkabaji Ibrahim Bance kutoka Marumo Gallants ya Afrika Kusini.

Kiungo huyo raia wa Burkina Faso anatajwa kuwa chaguo la kocha wa Simba, Steve Barker, ambaye anaamini ataongeza nguvu katika eneo la kiungo mkabaji ndani ya timu hiyo.

Barker anatafuta mbadala sahihi wa Allasane Kante, ambaye ameripotiwa huenda akapewa mkono wa kwaheri mwishoni mwa msimu.

Taarifa zinaeleza kuwa Bance anatarajiwa kumaliza mkataba wake na Marumo Gallants mwishoni mwa msimu huu, hali inayofungua mlango kwa Simba kumpata bila gharama kubwa akiwa kama mchezaji huru.

Iwapo mazungumzo hayo yatafanikiwa, basi Simba itakuwa imepata kiungo mwenye uwezo wa kukaba, kusoma mchezo na kusaidia ujenzi wa mashambulizi kutoka chini akishirikiana na viungo wengine.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’