Winga AFAD-Plateau katika rada za Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th May 2026


Winga AFAD-Plateau katika rada za Yanga

Klabu ya Yaanga imeingia katika mbio za kumsaka winga wa kulia wa klabu ya AFAD-Plateau, Amani Kouadiokan Michel Breygeneve (27), ambaye amekuwa na msimu bora nchini Ivory Coast.

Baada ya Ecua Celestin kushindwa kuwashawishi Wananchi na kupelekea akatolewa kwa mkopo JS Kabylie huku mbadala wake Buba Jammeh nae akishindwa kuingia kwenye kikosi cha kwanza, Yanga imejipanga kurudi sokoni kuimarisha eneo lake la washambuliaji wa pembeni.

Kwa mujibu wa taarifa za usajili, Yanga inafuatilia kwa karibu huduma ya mchezaji huyo ambaye amejipambanua kama mmoja wa wachezaji hatari zaidi katika ligi ya Ivory Coast msimu huu.

Breygeneve amekuwa katika kiwango cha juu akiwa miongoni mwa wafungaji bora, akifanikiwa kufunga mabao 10 na kutoa asisti 6 katika mechi 24 alizocheza msimu huu. Takwimu hizo zimemfanya kuwa miongoni mwa wachezaji waliovutia macho ya timu mbalimbali barani Afrika.

Mchezaji huyo anatajwa kuwa na uwezo wa kutumia miguu yote miwili, jambo linalomfanya kuwa tishio kwa mabeki wa pembeni. Aidha, anasifika kwa kasi na nguvu anazotumia anaposhambulia, sifa zinazomuweka kwenye daraja la wachezaji wanaoweza kutumika kwenye nafasi zaidi ya moja katika safu ya ushambuliaji.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’