Local,Yanga, Transfer News

Winga AFAD-Plateau katika rada za Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 May 2026
Winga AFAD-Plateau katika rada za Yanga

Klabu ya Yaanga imeingia katika mbio za kumsaka winga wa kulia wa klabu ya AFAD-Plateau, Amani Kouadiokan Michel Breygeneve (27), ambaye amekuwa na msimu bora nchini Ivory Coast.

Baada ya Ecua Celestin kushindwa kuwashawishi Wananchi na kupelekea akatolewa kwa mkopo JS Kabylie huku mbadala wake Buba Jammeh nae akishindwa kuingia kwenye kikosi cha kwanza, Yanga imejipanga kurudi sokoni kuimarisha eneo lake la washambuliaji wa pembeni.

Kwa mujibu wa taarifa za usajili, Yanga inafuatilia kwa karibu huduma ya mchezaji huyo ambaye amejipambanua kama mmoja wa wachezaji hatari zaidi katika ligi ya Ivory Coast msimu huu.

Breygeneve amekuwa katika kiwango cha juu akiwa miongoni mwa wafungaji bora, akifanikiwa kufunga mabao 10 na kutoa asisti 6 katika mechi 24 alizocheza msimu huu. Takwimu hizo zimemfanya kuwa miongoni mwa wachezaji waliovutia macho ya timu mbalimbali barani Afrika.

Mchezaji huyo anatajwa kuwa na uwezo wa kutumia miguu yote miwili, jambo linalomfanya kuwa tishio kwa mabeki wa pembeni. Aidha, anasifika kwa kasi na nguvu anazotumia anaposhambulia, sifa zinazomuweka kwenye daraja la wachezaji wanaoweza kutumika kwenye nafasi zaidi ya moja katika safu ya ushambuliaji.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’