Yanga yajipanga kumuongeza mkataba Dube

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th May 2026


Yanga yajipanga kumuongeza mkataba Dube

Habari njema kwa mashabiki wa Yanga ni kuwa uongozi wa timu yao umekamilisha mazungumzo ya awali ya kumuongeza mkataba mshambuliaji wake kinara, Prince Dube, katika juhudi za kuhakikisha anaendelea kubaki ndani ya kikosi hicho, imefahamika.

Dube ni miongoni mwa wachezaji muhimu katika kikosi cha Yanga ambao mikataba yao inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu, hali iliyolazimu klabu hiyo kuharakisha mazungumzo ya kumuongezea kandarasi mpya.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya klabu hiyo, pande zote mbili zimefikia makubaliano ya awali na kinachosubiriwa sasa ni hatua ya mwisho ya kusaini mkataba huo rasmi, hatua inayotarajiwa kufanyika muda wowote kuanzia sasa.

Uongozi wa Yanga umeamua kuchukua hatua hiyo baada ya kuridhishwa na kiwango cha mshambuliaji huyo ambaye amekuwa na mchango mkubwa katika safu ya ushambuliaji, akifunga mabao na pia kutoa pasi za mabao muhimu.

Dube kwa sasa ndiye kinara wa mabao ndani ya kikosi cha Yanga SC akiwa amefunga mabao tisa kwenye ligi, sambamba na kutoa pasi nne za mabao, takwimu zinazoonesha mchango wake mkubwa katika mafanikio ya timu hiyo msimu huu.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’