Local,Transfer News,Yanga

Yanga yajipanga kumuongeza mkataba Dube

Joel JJ By Joel JJ
β€’
7 May 2026
Yanga yajipanga kumuongeza mkataba Dube

Habari njema kwa mashabiki wa Yanga ni kuwa uongozi wa timu yao umekamilisha mazungumzo ya awali ya kumuongeza mkataba mshambuliaji wake kinara, Prince Dube, katika juhudi za kuhakikisha anaendelea kubaki ndani ya kikosi hicho, imefahamika.

Dube ni miongoni mwa wachezaji muhimu katika kikosi cha Yanga ambao mikataba yao inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu, hali iliyolazimu klabu hiyo kuharakisha mazungumzo ya kumuongezea kandarasi mpya.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya klabu hiyo, pande zote mbili zimefikia makubaliano ya awali na kinachosubiriwa sasa ni hatua ya mwisho ya kusaini mkataba huo rasmi, hatua inayotarajiwa kufanyika muda wowote kuanzia sasa.

Uongozi wa Yanga umeamua kuchukua hatua hiyo baada ya kuridhishwa na kiwango cha mshambuliaji huyo ambaye amekuwa na mchango mkubwa katika safu ya ushambuliaji, akifunga mabao na pia kutoa pasi za mabao muhimu.

Dube kwa sasa ndiye kinara wa mabao ndani ya kikosi cha Yanga SC akiwa amefunga mabao tisa kwenye ligi, sambamba na kutoa pasi nne za mabao, takwimu zinazoonesha mchango wake mkubwa katika mafanikio ya timu hiyo msimu huu.

More Stories

Manchester City yaichapa Sunderland 5–3 katika mechi ya mabao nane
Manchester City yaichapa Sunderland 5–3 katika mechi ya mabao nane
2h ago
READ MORE β†’
Atletico yang’ara kwenye dabi, Real Madrid aangukia pua ugenini
Atletico yang’ara kwenye dabi, Real Madrid aangukia pua ugenini
2h ago
READ MORE β†’
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
8h ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
10h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
12h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
12h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
13h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
13h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
14h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
21h ago
READ MORE β†’