Local,Transfer News,Singida

Singida BS yaanza na kinda mfungaji bora DR Congo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
7 May 2026
Singida BS yaanza na kinda mfungaji bora DR Congo

Klabu ya Singida Black Stars imeanza harakati za kuimarisha safu yake ya ushambuliaji kuelekea msimu ujao baada ya kuripotiwa kutuma ofa rasmi kwa klabu ya AS Dauphin Noir ya DR Congo kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji chipukizi, Candidat Mapendo.

Mapendo mwenye umri wa miaka 19, kwa sasa ndiye kinara wa mabao katika Ligi Kuu ya DR Congo (Linafoot), akiwa tayari amefunga mabao 22 msimu huu akiwa na AS Dauphin Noir.

Taarifa kutoka DR Congo zinaeleza kuwa Singida BS imeonyesha nia kubwa ya kumpata mshambuliaji huyo kutokana na kiwango chake bora cha ufungaji, kasi pamoja na uwezo wake wa kucheza ndani na nje ya boksi.

Hata hivyo, timu hiyo ya Tanzania inakabiliwa na ushindani kutoka klabu kadhaa za nje, ikiwemo timu kutoka Ureno ambazo pia zinamfuatilia kwa karibu nyota huyo chipukizi.

Mapendo amekuwa gumzo kubwa kwa timu yake katika Linafoot baada ya kuiongoza safu ya ushambuliaji ya AS Dauphin Noir kwa mafanikio makubwa. Katika michezo kadhaa ya ligi, amekuwa akiibeba timu yake kwa kufunga mabao muhimu, huku baadhi ya vyombo vya habari vya Congo vikimtaja kama mmoja wa washambuliaji bora wanaochipukia kwa sasa nchini humo.

Mbali na kuwa kinara wa mabao, mshambuliaji huyo pia ameweka rekodi ya kipekee kwenye ligi hiyo baada ya kuvunja baadhi ya takwimu zilizowahi kuwekwa na mastaa wa zamani wa soka la Congo akiwemo TrΓ©sor Mputu, kutokana na kasi yake ya kufunga mabao akiwa bado na umri mdogo.

Iwapo Singida BS itafanikiwa kukamilisha dili hilo, itakuwa moja ya usajili mkubwa wa klabu hiyo kuelekea msimu ujao.

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
2h ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
4h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
6h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
6h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
8h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
8h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
16h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
20h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
20h ago
READ MORE β†’