International,Normal News,Real Madrid, Barcelona

Mbappe aiwahi Barcelona, ashiriki mazoezi kujiandaa na El Classico

Joel JJ By Joel JJ
7 May 2026
Mbappe aiwahi Barcelona, ashiriki mazoezi kujiandaa na El Classico

Nyota wa Real Madrid CF Kylian Mbappé, ameripotiwa kuwa tayari kurejea uwanjani kuelekea mchezo mkubwa wa El Clásico dhidi ya FC Barcelonautakaopigwa Jumapili, May 10 baada ya kufaulu vipimo vya afya vilivyofanywa na madaktari wa klabu hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka COPE na vyombo vingine vya michezo vya Hispania, Mbappé ameonyesha maendeleo makubwa katika kupona majeraha ya misuli ya mguu wa kushoto yaliyokuwa yakimuweka nje ya baadhi ya michezo ya hivi karibuni ya La Liga.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alishiriki sehemu ya mazoezi ya pamoja na kikosi cha Real Madrid leo, jambo lililoongeza matumaini ya kuwepo kwake katika kikosi kitakachoivaa Barcelona kwenye mchezo huo mkubwa.

Mashuhuda kutoka mazoezini wamedai Mbappé alionekana akiwa na furaha na hali nzuri muda alipokuwa akiondoka kambini baada ya mazoezi, ishara inayotafsiriwa kuwa amejiandaa kurejea vitani katika kipindi muhimu cha msimu.

Awali kulikuwa na hofu kubwa kuhusu uwepo wake baada ya kupata majeraha kwenye mchezo dhidi ya Real Betis, hali iliyomfanya kukosa mchezo mmoja wa ligi huku akiendelea na programu maalum ya matibabu na mazoezi binafsi.

Hata hivyo, taarifa za sasa zinaonyesha benchi la ufundi la Real Madrid lina matumaini makubwa ya kumtumia nyota huyo dhidi ya Barcelona, mchezo unaotajwa kuwa muhimu kwa heshima ya Real Madrid ambayo haiko tayari Barcelona kutwaa ubingwa mbele yao.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
4h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
9h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
11h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
11h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
15h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
17h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →