Mbappe aiwahi Barcelona, ashiriki mazoezi kujiandaa na El Classico

Joel JJ By Joel JJ • 7th May 2026


Mbappe aiwahi Barcelona, ashiriki mazoezi kujiandaa na El Classico

Nyota wa Real Madrid CF Kylian Mbappé, ameripotiwa kuwa tayari kurejea uwanjani kuelekea mchezo mkubwa wa El Clásico dhidi ya FC Barcelonautakaopigwa Jumapili, May 10 baada ya kufaulu vipimo vya afya vilivyofanywa na madaktari wa klabu hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka COPE na vyombo vingine vya michezo vya Hispania, Mbappé ameonyesha maendeleo makubwa katika kupona majeraha ya misuli ya mguu wa kushoto yaliyokuwa yakimuweka nje ya baadhi ya michezo ya hivi karibuni ya La Liga.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alishiriki sehemu ya mazoezi ya pamoja na kikosi cha Real Madrid leo, jambo lililoongeza matumaini ya kuwepo kwake katika kikosi kitakachoivaa Barcelona kwenye mchezo huo mkubwa.

Mashuhuda kutoka mazoezini wamedai Mbappé alionekana akiwa na furaha na hali nzuri muda alipokuwa akiondoka kambini baada ya mazoezi, ishara inayotafsiriwa kuwa amejiandaa kurejea vitani katika kipindi muhimu cha msimu.

Awali kulikuwa na hofu kubwa kuhusu uwepo wake baada ya kupata majeraha kwenye mchezo dhidi ya Real Betis, hali iliyomfanya kukosa mchezo mmoja wa ligi huku akiendelea na programu maalum ya matibabu na mazoezi binafsi.

Hata hivyo, taarifa za sasa zinaonyesha benchi la ufundi la Real Madrid lina matumaini makubwa ya kumtumia nyota huyo dhidi ya Barcelona, mchezo unaotajwa kuwa muhimu kwa heshima ya Real Madrid ambayo haiko tayari Barcelona kutwaa ubingwa mbele yao.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →